Proverbs 13:1-6

Mema Ya Muda Mfupi Na Yale Ya Kudumu


1 aMwana mwenye hekima husikia mafundisho ya babaye,
bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.


2 bKutoka tunda la midomo yake mtu hufurahia mambo mema,
bali wasio waaminifu wanatamani sana jeuri.


3 cYeye alindaye midomo yake hulinda nafsi yake,
bali yeye asemaye kwa haraka ataangamia.


4 dMvivu hutamani sana na hapati kitu,
bali nafsi ya mwenye bidii
hutoshelezwa kikamilifu.


5 eMwenye haki huchukia uongo,
bali waovu huleta aibu na fedheha.


6 fHaki humlinda mtu mwadilifu,
bali uovu humwangusha mwenye dhambi.

Copyright information for SwhKC