Proverbs 13:1-6
Mema Ya Muda Mfupi Na Yale Ya Kudumu
1 aMwana mwenye hekima husikia mafundisho ya babaye,
bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.
2 bKutoka tunda la midomo yake mtu hufurahia mambo mema,
bali wasio waaminifu wanatamani sana jeuri.
3 cYeye alindaye midomo yake hulinda nafsi yake,
bali yeye asemaye kwa haraka ataangamia.
4 dMvivu hutamani sana na hapati kitu,
bali nafsi ya mwenye bidii
hutoshelezwa kikamilifu.
5 eMwenye haki huchukia uongo,
bali waovu huleta aibu na fedheha.
6 fHaki humlinda mtu mwadilifu,
bali uovu humwangusha mwenye dhambi.
Copyright information for
SwhKC